Mhe. Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Misri, Menejimenti, Watumishi Wenyeji wa Ubalozini na Wana Diaspora wote waishio nchini Misri wamepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Mhe. Ali Hassan Mwinyi - Rais wa Awamu ya Pili kilichotokea siku ya Alhamisi, Februari 29, 2024.
Tunamuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu ampe makazi mema Peponi. Amin