Tarehe 29-03-2026 Mhe. Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
nchini Misri Mej Jen. Richard M.Makanzo alikutana na Mhe. Lt.
Gen. Eng. Kamel Alwazeer, Naibu Waziri Mkuu wa Maendeleo ya
Viwanda na Waziri wa Uchukuzi katika ofisi yake iliyopo katika Mji
Mpya wa Serikali (NAC).
Dhumuni la kikao hicho ni juhudi za dhati za Mhe. Balozi za
kuhakikisha kuwa anatekeleza na kufuatilia masuala mbali mbali ya
ushirikiano katika sekta ya uchukuzi ikiwa ni sehemu ya kuimarisha
diplomasia ya Uchumi.
Katika yaliyojiri kwenye kikao kilichowakusanya wawili hao ni
pamoja na;
Utayari wa Serikali ya Misri katika kuanzisha mradi wa
“Shipping line” itakayotoa huduma baina ya bandari ya Safaga ya
nchini Misri na Bandaari ya Dar es Salaam. Mradi wa “Logistic
Centre” katika eneo lilolo karibu na bandari ya Dar es Salaam.
Kubadilishana uzoefu na utaalamu katika sekta ya usafirishaji na
mradi wa upanuzi wa bandari ya Da es Salaam.
Kwa upande wake Mhe. Balozi alimuhakikishia Mhe. Al Wazeer kuwa
Tanzania iko tayari kufanya majadiliano na Serikali ya Misri
kuhusu miradi hiyo. Aidha, alibainisha kuwa Bandari ya Dar es
Salaam ni moja ya bandari muhimu katika Afrika Mashariki, kwani
inahudumia takribani asilimia 90 ya biashara ya ndani ya Tanzania
ambapo huzingatiwa kuwa ni bandari muhimu kwa biashara katika eneo
hilo.
Katika kuhitimisha kikao hicho. Mhe. Balozi aliwasilisha salamu
kutoka kwa Mhe. Prof. Makame Mbarawa, Waziri wa Uchukuzi wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kusisitiza kuwa Tanzania ipo
tayari kwa ushirikiano kwa ajili ya maendeleo ya mataifa hayo
mawili.

